Hotline +255 768985500
Hotline +255 768985500
Benki ya Equity Tanzania imezindua rasmi Zanzibar Supreme, kituo cha huduma maalum za Equity bank kinacholenga kutoa huduma za kifedha zenye uzoefu wa hali ya juu, ushauri wa kibiashara na mahusiano ya karibu na wateja, kinachopatikana Kijangwani, Mjini Magharibi Zanzibar. Hii ikiwa ni hatua muhimu katika mkakati wa benki hiyo wa kuimarisha huduma za kifedha, kupanua ujumuishaji wa kifedha na kusaidia ukuaji jumuishi wa uchumi wa Zanzibar.

Naibu Waziri wa Fedha na Mipango wa Zanzibar, Dkt. Hamad Omar Bakari (katikati) kwa pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Equity Tanzania, Isabela Maganga (watatu kushoto) na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mjini Magharibi, Ali Maulid Juma wakizindua Kituo Kipya cha Zanzibar Suprime cha Benki ya Equity Tanzania, kilichopo eneo la Kijangwani, Zanzibar, Juni 6, 2026. Wengine pichani kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Biashara wa Benki ya Equity, Prosper Nambaya, Mkuu wa Wilaya ya Mjini, Dkt. Said Haji Mrisho, Mteja wa Benki ya Equity, Dkt. Issa Seif Pamoja na Meneja wa Kituo cha Zanzibar Suprime, Anas Ramadhan.
Uzinduzi wa Kituo cha Zanzibar Supreme unaongeza imani kwenye benki hiyo katika fursa za ukuaji wa uchumi wa Zanzibar pamoja na dhamira yake ya kuendelea kuhudumia wananchi, wafanyabiashara, taasisi na wawekezaji kwa karibu zaidi. Uzinduzi huu wa kituo cha Zanzibar Supreme uliongozwa na Mh. Dr. Hamad Omar Bakar, Naibu waziri wa Fedha na Mipango ambaye alikua ni Mgeni rasmi.

Kituo cha Zanzibar Supreme kimeanzishwa kwa lengo la kuhudumia wateja wa hadhi ya juu, wajasiriamali wakati na wa kubwa, kampuni, sekta ya hoteli, wawekezaji, pamoja na wadau wengine muhimu kupitia huduma za kibenki za kiwango cha juu, zenye kuzingatia mahitaji ya mteja na uhusiano wa karibu kati ya benki na mteja.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi huo, Mkurugenzi Mtendaji wa Equity Bank Tanzania, Bi. Isabela Maganga, alisema kufunguliwa kwa kituo hiki ni sehemu ya mkakati mpana wa benki hiyo wa kuwekeza katika huduma za kibenki zinazogusa sekta muhimu za uchumi na kuongeza upatikanaji wa huduma rasmi za kifedha.
“Uzinduzi wa kituo cha Zanzibar Supreme ni hatua muhimu katika safari yetu ya kuendelea kusogeza huduma za kifedha karibu na wateja wetu. Kupitia kituo hiki, tunalenga kutoa huduma za kibenki zinazokidhi mahitaji ya wateja binafsi, wafanyabiashara wa kati na wakubwa, kampuni, wawekezaji na sekta ya hoteli, ambayo ni moja ya nguzo muhimu za uchumi wa Zanzibar,” alisema Bi. Maganga. Aliongeza kuwa Equity Bank Tanzania itaendelea kuwekeza katika miundombinu ya vituo vya hudum kwa wateja, huduma za kidijitali, na suluhisho za kifedha zinazosaidia ukuaji wa biashara, uwekezaji, upatikanaji wa mitaji, na uwezeshaji wa kifedha wa muda mrefu. “Tunaamini kuwa taasisi za fedha zina jukumu muhimu katika kusaidia maendeleo ya kiuchumi kwa kutoa huduma zinazowezesha watu na biashara kushiriki kikamilifu katika uchumi rasmi. Kituo hiki ni sehemu ya dhamira yetu ya kusaidia ukuaji wa Zanzibar kupitia huduma bora, za kuaminika na zinazolenga mahitaji halisi ya wateja,” aliongeza uzinduzi huu pia unaendana na jitihada za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, kupitia Wizara ya Fedha na Mipango, za kuendeleza ukuaji endelevu wa kijamii na kiuchumi, kuongeza ushiriki wa wananchi na sekta binafsi katika uchumi, na kuwezesha mabadiliko chanya katika sekta za fedha na biashara kwa mwaka 2026 na kuendelea. Kituo cha Zanzibar Supreme kitatoa huduma mbalimbali za kibenki ikiwemo kufungua akaunti, huduma za mikopo, huduma za biashara, huduma za fedha za kimataifa, huduma za kidijitali, ushauri wa kifedha, na huduma mahsusi kwa wateja wanaohitaji uangalizi wa karibu na suluhisho za kifedha zilizoboreshwa. Hafla ya uzinduzi wa kituo hiki umewakutanisha viongozi wa Serikali, viongozi wa taasisi mbalimbali, wamiliki na watendaji wa hoteli, wafanyabiashara wakati na wakubwa, wawekezaji, wateja wa kimkakati na wadau wengine muhimu kutoka Zanzibar. Kwa kufunguliwa kwa Zanzibar Supreme, Equity Bank Tanzania sasa ina jumla ya matawi 19 nchini, hatua inayozidi kuimarisha uwepo wake na kurahisisha upatikanaji wa huduma za kifedha katika maeneo muhimu ya kibiashara na ukuaji wa uchumi. Mtandao wa matawi ya Benki unajumuisha Makao makuu / Golden Branch, Golden Supreme, Quality Centre, Kariakoo, Mwenge, Ubungo, Mbagala, Temeke na Nyerere jijini Dar es Salaam, pamoja na matawi yaliyopo Arusha, Mwanza, Dodoma, Moshi, Mbeya, Morogoro, Geita, Kahama na Zanzibar, ikiwemo kituo cha Zanzibar Supreme kilichozinduliwa rasmi.
Equity Bank Tanzania limited imeingia ubia na Klabu ya Simba katika kutoa kadi zenye chapa zao...
View MoreEquity Bank has today kicked off the issuance of Simba Fan Cards to over 20 million fans of the...
View MoreEquity Bank Tanzania has today handed over 5 mobile police posts to the Ministry of Home Affairs...
View MoreBenki ya Equity imezindua huduma za benki kwa njia ya kimtandao, huduma hizi zilizopewa jina...
View MoreThe new tax settlement avenue will be available for all TRA clients including non- Equity Bank...
View MoreEquity Bank Group, on Thursday announced that its profit after tax for the third quarter of 2014...
View MoreRegional financial services provider Equity Bank Group has returned to its traditional growth path...
View MoreEquity Bank Group’s investment in ICT and Focus on SME boosts profits by 11 percent in the year...
View MoreEquity Bank and American Express today announced a partnership agreement, through which Equity Bank...
View MoreThe approvals, which were secured during the firm’s 11th Annual General Meeting (AGM) held today...
View MoreRegional banking group, Equity Bank's reduction of interest rates by 700 bps from 25% to 18% has...
View MoreEquity Bank Group strengthens its fundamentals while expenses of ICT, Innovation and Product Rollout...
View MoreThe Group’s total assets posted a 24% growth during the year to close at Ksh 243 billion up from...
View MorePartnership to increase financial inclusion and boost EMV migration efforts in the region.
View MoreThe new identity is aimed at creating a sustainable growth path and service delivery in today’s...
View MoreEquity becomes the 1st bank in Eastern and Central Africa to achieve this milestone paving way for...
View MoreBecomes the first bank in Eastern and Central Africa to achieve the trillion-shilling balance sheet...
View MoreThe Award is conferred annually to exceptional individuals who exemplify their outstanding `business...
View MoreThe service presents the exciting prospect for the Tanzania community to receive seamless...
View MoreEquity Bank (T) leo imenzidua rasmi akaunti maalum ya utunzani fedha kwa kujiwekea kidogo kidogo ili...
ZaidiEquity Bank (T) imeahidi kuendelea kutoa elimu ya fedha na mikopo nafuu kwa vikundi vya uwekezaji na...
ZaidiCustomers with Equity Bank accounts can now transact seamlessly in any of the Equity Bank branches...
View MoreCustomers will have the freedom to execute forex requirements in real-time in a safe, convenient and...
View MoreEquity Bank Kenya Limited has received two International Standards Certifications - ISO 20000 and...
View MoreEquity Bank Tanzania has announced the appointment of Ms. Isabel Maganga as the new Managing...
View MoreEquity’s Eastern and Central Africa Recovery and Resilience plan is envisaged to provide financing...
View MoreEquity Group has eased its defensive strategy that had been deployed during the economic uncertainty...
View MoreThe partnership will champion the implementation of the Africa Recovery and Resilience Plan which...
View MoreDelegates from the United States of America (USA) have arrived in Dar es Salaam, Tanzania for a...
View MoreEquity Group Holdings Plc today reported Kshs.34.4 billion shillings profit after tax for the nine...
View MoreEQUITY GROUP REPORTS A RECORD KES 46.1B NET PROFIT AND A DIVIDEND PAYOUT OF KES 15.1B
View MoreNairobi Monday 13th May 2024… After reporting a 5% decline in profit after tax for the year ended...
Read MoreNairobi, Kenya, 3rd September 2024: Equity Group unveiled its third annual sustainability report for...
Read MoreNAIROBI, 12th November 2024: Against a backdrop of continued macroeconomic headwinds of high...
Read MoreNAIROBI, 27th March 2025: Equity Group Holdings Plc continues to deliver solid financial results,...
Read MoreNAIROBI, 29th May 2025: Demonstrating strategic agility and resilience in a dynamic global economic...
Read MoreEquity Group Holdings Plc has announced its Q3 2025 results, showcasing a robust performance driven...
Read MoreAsset Loan to Empower Women and Youth Entrepreneurs in Tailoring and Fashion Design Sector
Read MoreMwanza, Tanzania –Tarehe 24 Januari 2026. Benki ya Equity Tanzania, kwa ushirikiano na wadau...
Read MoreBenki ya Equity yazindua “wezesha account” akaunti ya amana ya muda maalum, inayolenga...
Learn MoreTanzania, Benki ya Equity imetangaza ushirikiano wa kimkakati na Mixx by Yas wenye lengo la kuleta...
Read MoreKatika kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani, Equity Bank Tanzania iliwaunganisha wanawake wateja na...
Read MoreBenki ya Equity Tanzania imezindua rasmi tawi jipya la Ubungo, lililopo ndani ya EACLC Mall (East...
Read More